1Daudi alimwimbia Bwana* maneno ya wimbo huu wakati Bwana* alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
2Akasema:
3Mungu wangu ni mwamba wangu,
4Ninamwita Bwana*, anayestahili kusifiwa,
5“Mawimbi ya mauti yalinizunguka,
6Kamba za kuzimu+ 22:6 Kuzimu kwa Kiebrania ni Sheol, maana yake ni Shimo lisilo na mwisho.* zilinizunguka,
7Katika shida yangu nalimwita Bwana*,
8“Dunia ilitetemeka na kutikisika,
9Moshi ukapanda kutoka puani mwake,
10Akazipasua mbingu akashuka chini,
11Alipanda juu ya kerubi akaruka,
12Alifanya giza hema lake la kujifunika:
13Kutokana na mwanga wa uwepo wake
14Bwana* alinguruma kutoka mbinguni,
15Aliipiga mishale na kutawanya adui,
16Mabonde ya bahari yalifunuliwa,
17“Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika;
18Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi,
19Walinikabili siku ya msiba wangu,
20Alinileta nje mahali penye nafasi tele,
21“Bwana* alinitendea sawasawa na uadilifu wangu;
22Kwa maana nimezishika njia za Bwana*;
23Sheria zake zote zi mbele yangu,
24Nimekuwa sina hatia mbele zake,
25Bwana* amenilipa sawasawa na uadilifu wangu,
26“Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu,
27kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu,
28Wewe huwaokoa wanyenyekevu,
29Wewe ni taa yangu, Ee Bwana*.
30Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi,
31“Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu;
32Kwa maana ni nani aliye Mungu
33Mungu ndiye anivikaye nguvu
34Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu,
35Huifundisha mikono yangu kupigana vita;
36Hunipa ngao yako ya ushindi,
37Huyapanua mapito yangu,
38“Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta,
39Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena;
40Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita;
41Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia,
42Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa;
43Niliwaponda kama mavumbi ya nchi;
44“Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu;
45nao wageni huja wakininyenyekea,
46Wote wanalegea,
47“Bwana* yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu!
48Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi,
49aniwekaye huru toka kwa adui zangu.
50Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana*,